Matthew 11:1-6
Isa Na Yahya Mbatizaji
(Luka 7:18-35)
1 aBaada ya Isa kumaliza kutoa maagizo kwa wanafunzi wake kumi na wawili, aliondoka hapo akaenda kufundisha na kuhubiri katika miji yao. 2 bYahya aliposikia akiwa gerezani mambo ambayo Al-Masihi ▼▼ Al-Masihi maana yake ni Masiya, yaani Aliyetiwa mafuta.
alikuwa akiyafanya, aliwatuma wanafunzi wake 3 dili wakamuulize, “Wewe ndiye yule aliyekuwa aje, au tumngojee mwingine?” 4Isa akajibu, “Rudini mkamwambie Yahya yale mnayosikia na kuyaona: 5 eVipofu wanapata kuona, viwete wanatembea, wenye ukoma wanatakaswa, viziwi wanasikia, wafu wanafufuliwa, na maskini wanahubiriwa habari njema. 6 fAmebarikiwa mtu yule asiyechukizwa na mimi.”
Copyright information for
SwhKC